Tabia 12 Chafu Za Mwanamke Ambazo Wanaume Hupenda


Hili chapisho limeandikwa spesheli kuonyesha tabia za mwanamke mtundu. Mwanamke mtundu hupendwa sana na wanaume. Je utawajuaje wanawake aina hii ama mwanamke atajijuaje kama yeye ni mtundu?


Hapa tumeweka tabia 12 za mwanamke mchafu ambazo kila mwanaume anazipenda.

#1 Mwanamke Mtundu.
Mwanamke mchafu si yule ambaye anajificha kuonyesha mambo yake anayoyafanya. Hawezi kujifanya kuwa hapendi kuangalia filamu za ngono, ama kuona haya/uoga wa kujaribu mitindo mipya ya kufanya mapenzi. Aina hii ya mwanamke huyafanya maisha ya mapenzi kwa mwanaume yeyote kuwa ya furaha na hakuna wakati yatakuwa yanaboa hata mara moja.

#2 Yuko sexy.

Vile ambavyo mwanamke anavaa kuna umuhimu sana. Kujifunika maleso nyakati zote ama kufaa nguo nzito nzito si vibaya kwa mwanamke, lakini pia fahamu kuwa kuna nguo ambazo mwanamke akivaa zitamvutia mwanaume.

#3 Anapenda kujaribu mambo mapya.

Mwanamke mchafu kawaida hajizuii kufanya mambo ambayo hajajaribu kufanya maishani.  Mwanamke kama huyu angependa kujaribu chochote kile hata kama ni mara moja. [Soma: Jinsi ya kumtongoza mwanamke ambaye hamko ligi moja]

#4 Wanapenda kusuka.
Wanawake wachafu wanaijua sanaa ya kutongoza na kutumia lugha ya ushawishi kwa mwanaume yeyote bila wao kuonyesha azima ya kufanya hivyo. Ni wanawake ambao wanafurahisha, wanajua kutumia maujanja na kuzungumza utamu kimapenzi. Wanaweza kumfanya mwanaume yeyote kupandwa na hisia za mapenzi bila hata kuwagusa.

#5 Anasimama kujitetea yeye mwenyewe.

Mwanamke huyu kwa kawaida anajiamini yeye mwenyewe na kwa kawaida atafanya juu chini kuhakikisha lile ambalo analotaka kutimiza limetimia. Hatazuiwa na yeyote yule. Yeye hatahitaji usaidizi kutoka kwa mwanaume yeyote ili kufanikisha azma yake.

#6 Yeye ni yeye.

Mwanamke aina hii hahitaji aitikie yale ambayo yanahitajika katika jamii. Si lazima ya yeye kujitweka majukumu ama kufuata masharti na sheria za jamii. Anajua kuwa wengine wanamjua.

#7 Hapaki mafuta kwa mgongo wa chupa.
Mwanamke wa kawaida atamshika mwanaume mkono na kumwambia kuwa kila kitu kiko sawa ilhali mambo yanaharibika. Mwanamke mchafu yeye haogopi kukabiliana na ukweli, kama kuna tatizo atamwambia ukweli mwanaume ili tatizo kama hilo walitatue.

#8 Ni mwanamke ghali kumtunza.

Wanaume wangependa huwa na wanawake ambayo ni rahisi kwao kuwatunza.? Lakini ndani yao huwa wanatamani kum-maintain mwanamke ambaye ni ghali zaidi. Ukweli ni kuwa kila mwanaume ndoto yake ni kuona kuwa ana mwanamke ambaye anatumia hela nyingi kutoka kwake hata kama hana uwezo kama huko.[Soma: Maswali 20 machafu ya kumuuliza mwanamke Whatsapp mpaka apandwe na nyege]

#9 Wanawake wachafu hawajiachilii hivi hivi.
Wanawake wengi wa kawaida mara nyingi hujiachilia pindi wanapoingia katika uhusiano mrefu na mwanaume.  Hii inamaanisha kuwa wanaacha tabia za kawaida za kujipodoa na kujirembesha. Baada ya muda utapata kwamba amejiachilia kiasi cha kuwa anaanza kuwa na mafuta mengi mwilini...wanakuwa kama kile kibonzo cha Michelin Tyres. Kwa wanawake wachafu, hii ni kinyume yake kwani hakuna siku atasahau make up wala vipodozi.

#10 Wanasema "SITAKI"
Wanaume hawapendi kusikia mwanamke yeyote akichukua misimamo mikali kwao. Lakini baada ya muda flani atachukuliwa kuwa ni mwanamke asiyetaka kuchezewa. Na wakati wote yeye yuko serious na mambo yake. Mwanamke wa kawaida kwa kuwa hataki kumkosea mwanaume anabakia kukubali chochote kile ambacho ataambiwa na mwishowe kufanywa zuzu ama kuchezewa na mwanamume.

#11 Hangojei miujiza itendeke.
Yeye ndio hufanya hio miujiza. Hawezi maisha yake yote kungojea yule ambaye atakuja kumtatulia shida ama matatizo yake. Aidha yeye atapambana na dunia kuhakikisha kuwa ametatua matatizo yake, akiwa na usaidizi wa mwanaume yeyote ama yeye mwenyewe.[Soma: Aina 12 ya wanawake ambayo watayafanya maisha yako kuwa magumu]

#12 Anajiamini kupindukia.
Mwanamke huyu anajiamini kupindukia kiasi cha kumfanya mwanaume kuingiwa na woga wa kutaka kumridhisha zaidi. Chochote atakachofanya huwa anajiamini na kila mtu anamheshimu kwa aina ya tabia hio.

Well, hapo juu ni baadhi ya tabia ambazo zinamfanya mwanamke mchafu kuwapendeza wanaume. Kujiamini na kujifahamu ndio mpango mzima ambao mwanamke huyu anatumia ili kuitawala himaya yake. 


No comments:

Jiunge na jamii yetu ya Facebook/App yetu ili uweze kutangamana na members na readers wetu wa Nesi Mapenzi ama ujitafutie mpenzi HAPA

Powered by Blogger.
##valentine ##valentine