Jinsi Ya Kuanza Mazungumzo Na Mwanamke


Wanaume wengi hutaka kujua jinsi ya kuanzisha maongezi na mwanamke, mara nyingi hutokea iwapo mwanaume ni mwoga ama mwenye aibu.

Jambo hili hawawezi kulihepa kwa sababu kuongea na mwanamke ni jambo moja la lazima ambalo mwanaume yeyote anapaswa kutimiza. So utafanya nini iwapo hujua kuanzisha ama kuongea na mwanamke?

Jibu tunalo kwa sababu tumekuandalia mbinu tofauti tofauti ambazo unaweza kuzitumia ili kuanzisha gumzo na mwanamke.

Kuanzisha gumzo na mwanamke

1.Mchokoze
Ingawaje hungependa kuanzisha majibizano ama ugomvi na mwanamke, ni vizuri kutumia mbinu hii kwani inaleta matokeo ya juu. Mada utakayochagua wakati wa kuongea kwako kutategemea na ujasiri wako na pia mazingara yako.  Unaweza kuanzisha mada ya kuhusu msanii anayempenda, filamu aliyoiangalia ama mambo mengine. Akiwa anakujibu, wewe tingisha kichwa chako halafu ucheke polepole. Hii itamfanya audhike. 

2. Muulize maoni yake
Kila mtu anakuwa na maoni yake kuhusiana na maswala tofauti tofauti. Hii ni mbinu ambayo ni rahisi na ambayo hutumiwa sana kuanzisha mazungumzo. Kama hujui kitu cha kumuuliza basi tumia mazingira ambayo uliopo wakati huo. Mfano kama uko na yeye katika supermarket, unaweza kujaribu kumuuliza kuhusu kati ya sukari ya kampuni flani na nyingine gani ni bora. Hii haitatumika kama mchongo pekee, bali pia kama ni mwanamke ambaye anapenda kusocialize atapenda maongezi yako. [Soma: Kumpandisha nyege mwanamke kwa kukaa kando yake]

3. Muulize maoni kuhusu mahusiano
Iwapo unataka kujua hisia za mwanamke ikija na maswala ya mahusiano, bila kuonekana kama tishio lolote, basi jaribu kutumia mbinu ya kumuomba ushauri unaohusiana na maswala ya mahusiano. Jaribu kumwonyesha ya kuwa ushauri huo unaotaka si wa kwako bali unajaribu kumuulizia rafiki yako. Mchokore vizuri na ukifaulu, jaribu kumuuliza kuhusu mahusiano yake aliyopitia na kumuuliza mambo mengine bila kuonekana kama tishio kwake wala kuona ya kuwa unamuuliza haya yote kwa sababu zako binafsi.
Kila mtu anakuwa na maoni yake. Hivyo kumuuliza mwanamke ushauri kuhusiana na mahusiano atakuona umemthamini na msaidizi wakati uo huo.

4. Tumia mchongo wa chakubimbi
Wanaume wengi hupenda kutumia michongo wakati wanapotaka kuongea na mwanamke. Well, mbona usitumie michongo aina tofauti na wanaume wa kawaida? [Soma: Aina ya michongo inayotumiwa kuanzisha gumzo na mwanamke]
Ukiona mwanamke ambaye unataka kuongea naye, msogelee karibu yake halafu umwambia "Kusema ukweli naona ya kuwa kila mwanamke huwa anapenda" Ukimwambia hivi bila shaka atasogea mbali na wewe. Kama ameweza kuula mtego wako, basi atakuapproach na kutaka umweleze ulikuwa unamaanisha nini ulipomwambia hivyo. Uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa unauhakika ya kuwa mwanamke kama huyu amekuwa intrested na wewe bila kuchukua hatua nyingine.


Owk. Wanaume wengi wakati mwingine huingiwa na uoga wa kutaka kuongea na baadhi ya wanawake lakini kwa kutumia baadhi ya hizi mbinu tulizoziorodhesha hapo juu, mambo yako yanarahisishwa kirahisi.


1 comment:

Jiunge na jamii yetu ya Facebook/App yetu ili uweze kutangamana na members na readers wetu wa Nesi Mapenzi ama ujitafutie mpenzi HAPA

Powered by Blogger.
##valentine ##valentine