Jinsi Ya Kuwasiliana Na Wanawake Na Mbinu Ya 'Wapatanishi Mateka'


Ok najua ushawahi kuona jambo kama hili katika sinema si mara moja wala mara mbili...

Majambazi waliobanywa ambao wamevamia benki wakiwa ndani na bunduki zao huku wakitishia kuua mateka wao...

Ama jamaa ambaye amekumbwa na misongo ya mawazo (stress) amesimama katika ncha ya ukuta wa jumba lenye ghorofa 30 na anatishia kujirusha...

Hatua aina hii utapata polisi wakimuita mtu mahususi aka mpatanishi ambaye atahitajika kuongea na watu aina hii kwa amani bila kutokea jambo lolote baya...

Watu hawa huwa wamefundishwa spesheli kutatua aina hii ya migogoro na hakuna anayeweza kuwashinda kwa ujuzi wao dunia hii. Wanajua jinsi ya kutumia maneno na lugha MAHUSUSI ambayo itamfanya mtu kusisimka kihisia na kuweza kuwakontrol vile ambavyo wanataka wao.

Wanayajua maneno ambayo yanafanya kazi kama hirizi ambayo yatamfanya mtu kutulia na kumfanya aamini kila kitu ambacho ataongea.

So, je mbinu hii unaweza kuitumia kwa mwanamke?

Mbinu hii mwanzo ni rahisi sana kuitumia kwa mwanamke. Hii ni kwa sababu mara ya kwanza unapokutana na mwanamke na kuanza kumuongelesha huwa hajiskii huru na uwepo wako, huwa kwa kawaida anajiskia kama wewe uko hapo na unamtatiza shughli yake ambayo alikuwa akifanya. So kitu cha kwanza cha kufanya huwa unajaribu kumuonyesha kuwa wewe ni mtu salama na unaomba muda wake kiasi uongee naye (inajirudia katika hali ya mtekaji nyara na mpatanishi)

Zama nami...

Ok mwanzo nafaa nianze kwa kueleza hivi kwa wale ambao hawajajua mbinu hii.

Kuna kitu ambacho huwa kinatokea katika situation ya utekaji nyara: Watekaji nyara kwa kawaida huwa na hofu mwingi muda wote. Kwa kawaida hukumbwa na misongo ya mawazo muda wote ambao watakuwa na mateka wao.

Hii ni kama vile mwanamke anapopandwa na misongo ya mawazo asiyoweza kuizuia wakati wowote ambao mwanaume asiyemjua anamuapproach na kuanza kumtongoza.

So katika hali kama hii, unapaswa kujua jinsi ya KUONDOA misongo yake ya mawazo na UJENGE MSHIKAMANO na yeye haraka iwezekanavyo.


Unapaswa kutumia maneno yafaayo ambayo yatamfanya apumzike na kutulia...

Na kufanikisha haya yote hupaswi kutumia maneno ambayo yanachosha kama vile...

"Hivi wewe waitwa nani?"
"Ushawahi kuwa hapa awali?"
"Unafanya kazi gani?"

....na maneno mengine aina hii ambayo yanachosha.

Hapa lazima utumie maneno ambayo yatakuwa kama kitufe ambacho ukikifinya tu atakufungukia na kukuambia kila kitu ambacho unataka aseme...

Na unayavuta maongezi yenu mbali na 'sehemu hatari' ambazo zinaweza kusababisha yeye kupoteza hamu na wewe (90% ya wanaume hufanya MAKOSA HAYA ya kuleta mada ambazo zinawaudhi wanawake...)

Na wakati uo huo, unaingiza mbinu na maujanja rahisi ambayo yatachangamsha hisia chanya na kuondoa ukinzani wowote...

Kwa lugha nyepesi namaanisha ya kuwa lazima ujue jinsi ya kucontrol

Zifuatazo ni baadhi ya hali na jinsi ya kuzitatua...

Hali: Unataka kumtoa out mwanamke lakini hujui ni vipi atareact.

Mbinu: Watekaji nyara huwa wanapenda kuhakikishiwa usalama wao iwapo watajisalimisha kwa amani. Hivyo mpatanishi huelezea kabisa yale yote ambayo yatakayojiri baada ya kujisalimisa ili kuondoa woga wowote.

Atasema hivi: Nataka tu ujue Papito, kama utajitokeza na kuongea na mimi, hakuna mtu atakutatiza. Ni mimi na wewe tu ambao tutaongea...hakuna cha zaidi.

Vivyo hivyo kwa mwanamke, unafaa kumwambia yatakayojiri. Bila hivyo atakuwa akijiuliza ni KITU GANI ambacho kitakachotokea akikubali mwitikio wako wa kutoka out na wewe.

(Je unajaribu kuingia katika chupi yake? Ama wataka kumpeleka katika sehemu ambayo itamboa na ambayo haitamstarehesha? Ni kitu gani ambacho kitatokea kati yako na yeye??)

Mwambie hivi: "Nataka kukupeleka katika huu mkahawa/klabu ambayo niliivumbua hivi karibuni... ni sehemu nzuri ambayo naamini utaipenda kwa sababu wanacheza nyimbo nzuri na za kuvutia, mwanzo sehemu hii inalingana na ladha yako. Ntakuwa huko usiku wa Ijumaa, mbona tusiende pamoja na wewe wakati wa saa tatu usiku? Huwa sipendi kuchelewa sana nikiwa nje usiku lakini nikiwa na wewe nitaspend muda mrefu kiasi na wewe ili tujiinjoy zaidi...."

Hapa utakuwa ushaeleza matokeo yote yatakayojiri akiwa na wewe usiku huo.

(Kwa kutumia mbinu hii, utakuwa ushamjulisha matokeo yote ambayo yatatokea USIKU HUO kimukhtasari, lakini utakuwa umeweka plan yako kwa njia ambayo inaonekana ni nzuri na ambayo haimtishii. Utakuwa umerahisisha kwake kukubali na kusema "ndio")

******

Hali: Anaendelea kuzidi kukutajia kuhusu ex boyfriend wake, na kila wakati akimtaja anaharibu hisia za mazungumzo.

Mbinu: Mfanye ex boyfriend wake asionekane na thamani yeyote na 'kuziondoa nguvu zake zote' kwa  kumrejelea kama "yule mwanaume"...halafu unajeuza mada mliokuwa mkiongea.

Mfano...

Wewe: "Unajua Mamito, inaonekana kama YULE MWANAUME kiukweli hakuwa katika level yako hivyo ilikuwa jambo zuri kuachana naye. Nahisi kuna mengine muhimu zaidi ambayo yanakufaa kumliko...hebu niambie zaidi kuhusu kazi yako, naona inavutia zaidi kuona kuwa wewe ni (TAJA KAZI ANAYOFANYA)"

Wapatanishi hutumia mbinu ii hii wakati wanapotaja 'bunduki' ama 'bomu'...hakuna wakati watasema "Nataka uishushe bunduki yako," hii ni kwa sababu hilo NENO MOJA litamsisimua mtekaji nyara na kuongeza levels zake za stress.

Badala yake, wao husema "Ni mimi na wewe pekee tunaoongea, Papito, so nataka utulie na uweke HICHO KITU chini..."

(Na kufanya hivi wanaanza kuongea kuhusu maswala mengine ambayo yanajenga mshikamano wa nguvu...)

Psss...soma (sehemu ya pili ya chapisho hili)



No comments:

Jiunge na jamii yetu ya Facebook/App yetu ili uweze kutangamana na members na readers wetu wa Nesi Mapenzi ama ujitafutie mpenzi HAPA

Powered by Blogger.