Mwanamke Mwenye Uchu Utamjuaje? Ishara Zote 12 Tunazo



Je unamjua mwananamke mwenye kiu? Kama unamjua ni mwanamke gani basi swali la pili unafaa ujiulize ni je yule mwanamke ninayemfukuzia ni mwenye kiu au la?

Najua ushawahi kuskia aina hii ya mwanamke lakini huzijui tabia zake, labda hujawahi kukumbana na mmoja ana kwa ana. Well, leo sifa zake tutaziorodhesha. Huyu ni mwanamke ambaye huwa na sifa za uchu, ni rahisi kumuapproach na kukupa uroda bila kufikiria mara mbili.


Kama unataka kujiridhisha haraka basi hawa ndio wanawake unaweza kuwafukuzia na utakuwa na uhakika wa juu ya kuwa utafaulu katika azma yako. Lakini iwapo unataka mwanamke wa kumpeleka nyumbani kwenu na mwishowe kumuoa basi epuka na aina hii ya mwanamke.

Mwanamke mwenye kiu na uchu utamjua na tabia zifuatazo.

#1 Ulimpata katika baa/klabu.  Hapa sisemi kuwa wanawake wazuri hawapatikani katika baa ama vilabu, la. Ninachosema ni kuwa ukipata mwanamke sehemu hizi halafu baada ya usiku mwingi kuingia anakubali kwenda na wewe nyumbani kwako basi ujue ni mwenye kiu. Labda lengo lake kuu ilikuwa nikuenda klabu na kupata mtu wa kulala naye.

#2 Alikuwa amekujaajaa. Hii ni njia ya moja kwa moja kuonyesha kuwa mwanamke aina hii anajionyesha ili umchague. Mwanamke ambaye anataka mahusiano ya kweli hawezi kuwa na hisia za kukushika ama kukuingia mwilini wakati wote. Mwanamke mwenye kiu atafanya hivi ili akuvutie umpende haraka.

#3 Ulilala na yeye haraka. Kuna wanawake wengi ambao wanaweza kuingiliana haraka na wewe halafu wakaendelea na mahusiano marefu, lakini mara nyingi wanawake hawa huwa wanataka tu kula uroda. Wana kiu cha kutambulika na pia kutaka zaidi. Wanawake wengi hudhania kuwa kulala na mwanaume ni njia ya kumfanya akutambue haraka, jambo ambalo si kweli.

#4 Anakupigia simu usiku wa manane. Hii hufanyika iwapo mwanamke ana uchu na wala hana lengo la kuwa katika mahusiano. Wanawake aina hii watakupigia usiku wa manane ili watimize tamaa zao za uchu. Ukiwaambia waje kwako nyakati hizo za usiku watakuja mara moja.

#5 Mawasiliano yenu ni ya mlalano.  Kiufupi mahusiano yenu ni ngono, ngono, ngono. Hata kama mmeenda out kuangalia filamu mwisho wa siku mtafanya ngono. Hakuna cha ziada ambacho mtakuwa mnaongea. Hii ni ishara kuu ya kutambua iwapo mwanamke huyu ana kiu kisichoisha.

#6 Anataka kujua kila kitu kukuhusu. Hapa mwanamke aina hii hatakupa time. Ana tamaa ya kukufahamu kila kitu kwa lengo la kuingia katika mahusiano na wewe. Atakuwa anakuuliza maswali yasiyokuwa na mwisho. Epuka mwanamke kama huyu sababu kiu chake kukimaliza si rahisi.

#7 Anasuka kila mwanaume anayemuona. Utamjua ni mwanamke mwenye kiu kwa kuwa anatafuta atenshen. Ni kama ana njaa isiyoisha hivyo kila mwanaume atakayekutana naye atakuwa anarusha ishara za kutongoza hata kama unatembea ama uko na yeye.

#8 AnakuSMS kwa mpigo bila kusita. Aina hii ya mwanamke atakuwa anataka kuwasiliana na wewe kila wakati. Ukiona mwanamke anakutumia meseji mara kwa mara, kila wakati basi fahamu anataka atenshen. Kiu chake kwako bado kiko kingi.

#9 Anasema kuwa nyinyi ni wapenzi mara ya kwanza kuongea naye. Hata kama uko mshapu kiasi gani katika kutongoza wanawake, ukiona ya kwamba mwanamke anajitokeza na kujitambulisha kuwa wewe na yeye mko pamoja na hata hujapiga hatua ya maana kumtongoza basi hapo fahamu kuwa kuna tatizo. Itakuwa ni wale aina ya wanawake wanaotaka kuonekana kama wana wapenzi. Huyu ni mwanamke mwenye kiu cha kuwa na uhusiano bila hata kufikiria.

#10 Anakuashiria maneno ya mapenzi. Labda mnaongea tu mambo ya kikawaida halafu ghafla mwanamke aina hii akaanza kukutajia maswala ya mambo anayopenda kitandani, filamu za ngono, uroda nk bila hata kufikiria. Well, huyu atakuwa anarusha nyavu kuangalia kama itanasa chochote. Hapa ukizubaa tu utanaswa, na kiu chake hakitamalizika.

#11 Anahakikisha anakuona mara kwa mara. Kila wakati yeye anapiga mahesabu ya sehemu ambazo anaweza kukutana na wewe mpaka inafika mahali unaudhika. Well, huyu ni mwanamke ambae kiu chake bado hakijakamilika vilivyo.

#12 Yuko rahisi. Si kila mwanamke ambaye utakumbana naye atakuwa rahisi kumtongoza. Na si kila mwanamke unayelala naye kirahisi anaweza kuingia katika mahusiano marefu na wewe. Lakini ukiona kuwa huyu mwanamke anakufungulia chupi haraka, utahitaji uwe na tashwishi na unahitajika kumchunguza zaidi iwapo ataonyesha ishara tulizoziorodhesha awali kuhakikisha kuwa ni mwanamke mwenye uchu.

Well, je wataka kuwajua na kuwatambua aina hii ya wanawake? Kitabu chetu cha Kutongoza Mwanamke: Kuanzia Hadharani Hadi Kitandani kitakufundisha na kukuelekeza.



No comments:

Jiunge na jamii yetu ya Facebook/App yetu ili uweze kutangamana na members na readers wetu wa Nesi Mapenzi ama ujitafutie mpenzi HAPA

Powered by Blogger.
##valentine ##valentine