Siri 15 Za Kumfanya Mwanamke Yeyote Akupende


Kutongoza mwanamke wakati mwingine inaweza  kuwa na tatizo. Hizi hapa ni mbinu na ujanja 15 za jinsi  ya kutongoza wanawake na wafall na wewe.

Tumeshapitia hapo. Kuna yule mwanamke mrembo ambaye umekufia naye na unahamu ya kutaka kumjua. Lakini kuna lile tatizo linajitokeza ambalo linakufanya ushindwe kuongea na yeye uso kwa uso. Unatamani kuwa na uwezo wa kumuapproach ili umsome akili yake na umwambie yale yote yaliyo moyoni mwako.


Hapo hapo, ijapokuwa kutongoza mwanamke huwa inakuja automatic kwa baadhi ya watu, kwa wengine inawafanya wajihisi wako katika hali ngumu. Yale mawazo tu ya kumuapproach mwanamke yakiwajia wanaanza kutokwa na kijasho kwa mikono, midomo inakauka, na unaanza kuongea kama kigugumizi unapotamka maneno – yaani inakuwa mbaya kujieleza na si vizuri itokee kwa mwanaume yeyote.

Habari njema ni kuwa unaweza kujifunza njia za kutongoza, na ufanye mazoezi ya kutongoza hadi ujihisi kuwa umejiamini na tayari kuandama msichana unayempenda. Na kwa hilo, tumekuja na mbinu 15 ambazo unaweza kuzitumia kutongozea wanawake.

#1 Tabasamu. Kutabasamu ni hatua ya kwanza bora ya kuanzia, haswa wakati ambapo umeingiwa na kibaridi. Hakikisha ya kuwa anayaangalia macho yako na unamaintain mtizamo wa macho yenu. Tabasamu huku unajiamini na usiwe wa kwanza wa kuangalia kando.

Kama atakurushia tabasamu, basi angalia kando kwa dakika chache halafu mwangalie tena huku ukitabasamu. Njia hii itampa ishara ya kumwambia kuwa uko interested na yeye. Lakini usifanye kosa la kurudia rudia kumtabasamia kwa sababu atakuona kama fala. So unachohitajika ni kujiandaa kumuapproach ili uanze mazungumzo.

#2 Tumia miondoko ya mwili inayofaa. Hakikisha unamakinika na miondoko ya mwili wako wakati unapozungumza na yeye. Kama umeingiwa na wasiwasi, usitie shaka muaproach mwanamke huyu kana kwamba hauko interested na yeye. Kuikunja mikono yako, kuangalia miguu, na kuangalia kando hupaswi kufanya kamwe.

Kuwa wazi na utumie macho yako kuwasiliana naye – mwangalie bila kuona aibu! Tumia mwili wako kumtongoza. Mwonyeshe kuwa umevutiwa na yeye.

#3 Mguse. Njia rahisi ya kumtongoza mwanamke ni kumgusa. Unaweza kumsugua na mkono wako, ama kama umekaa kando yake unaweza kuuachilia mguu wako umguse. Iwapo amependezwa na wewe hatauondoa.

Kama unamjua zaidi, kumgusagusa hua inafanya kazi vizuri sana. Mkumbatie, weka mkono wako kiunoni mwake wakati unaongea na yeye na hali kadhalika. Fanya haya yote iwapo tu hakatai. Na ukiona kama anarudia kile ambacho unamfanyia basi ujue umefaulu.

#4 Mfanye acheke. Ucheshi ni kitu cha kwanza ambacho wanawake huangalia kwa mwanaume, hivyo basi ni lazima ujifunze tabia ya kuwa mcheshi kama unataka kufaulu katika sanaa ya kutongoza. Kama unaweza kumchekesha basi utamfanya ajifeel amerelax na wewe mara moja hivyo kumvutia.

Si lazima uwe mcheshi kama Kingwendu ama Churchill ili umfanye acheke, la. Kinachohitajika ni uwe mhalisi. Kila mtu katika huu ulimwengu ana kipawa chake cha ucheshi. Hivyo unaweza kukumbuka jambo lolote ambalo ushawahi kuchekesha mtu. Mwanamke akikupenda anaweza kuchekeshwa na kila neno ambalo utasema.

#5 Mwache aombe nguo zako. Anapenda kuvalia lile vagazi lako kubwa, so mpatie avae kama kuna baridi. Hakikisha pia linanukia marashi yako, na kama anakupenda, atatamani akae nalo ili alikumbatie kwa kitanda na akuote katika ndoto zake.

#6 Msifu. Kumsifu mwanamke huwa ni mbinu nzuri ya kutumia wakati unapotongoza mwanamke, so mwonyeshe kuwa anavutia. Kama hutaki kwenda haraka unaweza kuanza na maneno kama ‘leo unapendeza’ ama ‘nimependezwa na kiatu chako’. Hii ni njia ya rahisi kumwambia mwanamke kuwa anavutia bila kusema neno ambalo litamuudhi.

#7 Kuwa mzuri mbele ya marafiki zake.  Hakikisha kuwa unajipa time na marafiki zake. Kama ataona kuwa unajaribu kuwasiliana na marafiki zake, itampa ishara kwake kuwa umependezwa naye na uko tayari kuspend muda naye. Kama bado hajaamua basi atatafuta ushauri kutoka kwa marafiki zake na itakuwa rahisi kwao kukuidhinisha kwake.

#8 Muulize maswali.  Kama unataka kujua kutongoza wanawake basi lazima uonyeshe interest kwa kumuuliza maswali mengi.

Atashukuru ule muda wote ambao umekaa na yeye ukimuuliza maswali kutaka kumjua zaidi. Hakikisha unamakinika na majibu yote ambayo atakwambia ili wakati mwingine mtakapokutana  usisahau chochote kile wakati ambapo atakuuliza swali.

#9 Ijue familia yake. Kuijua familia yake ni njia nyingine ya kuonyesha kuwa umevutiwa na yeye na uko tayari kujipa muda kujua zaidi kumhusu.

#10 Mfanyie favour/fadhila. Kutongoza mwanamke huwa kunakuja na njia tofauti tofauti. Kumwonyesha ukarimu mwanamke kwa kumfanyia jambo asilotarajia ni njia murua ya kuhakikisha kuwa utawini penzi lake.

#11 Mnunulie kinywaji.  Wakati mwingine vile vitu rahisi huwa ndivyo bora. Kama unataka maongezi yenu yawe rahisi na yaliyotulia basi huna budi kumnunulia kinywaji halafu mazungumzo yaanze na hapo.

#12 Mnunulie zawadi.  Zawadi nzuri na yakuvutia ni njia nzuri ya kumtandaza mwanamke katika hali ya kumtongoza. Unaweza kumzawadia zawadi cheshi na yakufurahisha haswa kutokana na mambo ambayo ameyataja kutokana na mazungumzo yenu ya awali. Hii itamvutia. Hakikisha haumnunulii zawadi ambayo ni ya gharama ama iliyo serious coz unaweza kumuogopesha.

#13 Kuwa interested na mambo anayopenda. Pata kujua kile kitu anachopenda na kufanya wakati yuko free, vitu anavyopenda na kila kitu. Hii itakupa nafasi ya kuwa na mambo mengi ya kuongea kuhusu. Ataona kana kwamba mnafanana kimtizamo flani.

#14 Mtumie SMS. Mazungumzo ya SMS ni njia nzuri kwa kutongoza. Kwa mtu mwenye kuona aibu inakuwa rahisi kwake kabla ya kuanza mazungumzo ya moja kwa moja. Mtumie jumbe za kutongoza, cheshi, na kama atajibu inavyostahili unaweza kumtumia jumbe zaidi.

#15 Mtese.  Kumtesa kwa upole ni njia nzuri ya kuanza kutongoza mwanamke. Kila mtu anajua kuwa wale wavulana wadogo hupenda kuvuta nywele za wasichana wadogo ambao wamependezwa nao. Hivyo hivyo kumtatiza mwanamke kwa upole, unampa ishara kumwambia  kuwa umevutiwa naye. Hii mbinu ina utata lakini ni kweli.

Mbinu ndizo hizi tushakupa. Usingojee tena. Zima simu uanze kumuapproach yule dada sahizi!

No comments:

Jiunge na jamii yetu ya Facebook/App yetu ili uweze kutangamana na members na readers wetu wa Nesi Mapenzi ama ujitafutie mpenzi HAPA

Powered by Blogger.