Ishara Za Kuonyesha Kuwa Mwanamke Anataka Umfukuzie


Katika Sanaa Ya Kutongoza, mwanaume huwa ndie anapaswa kumuaproach  mwanamke . Na katika mchakato huo huwa kuna mambo mawili ambayo anatarajia: unaweza kutumia nguvu zako zote kwake mpaka akakuona kuwa wewe ni mtu mlafi wa mapenzi na akakutoroka. Na pia ukienda polepole kwake anaweza kukuambia kuwa wewe ni mzembe wa mapenzi. Huna mshiko wa kuonyesha kuwa una haja ya kupenda. Kwa mambo haya mawili, wanaume wa kazi husema, “Wanawake, kuweni na msemo thabiti, hatutaki kuzungushwa.”

So hivi ni kweli kuwa wanawake wanapenda kufukuziwa?

Jibu ni ndio. Lakini kueleza kimahususi ni kuwa wanawake wanapenda kufukuziwa na wanaume ambao wameteka interest ama hisia zao. Kwa wanawake inakuwa rahisi kuwavutia wanaume bila tatizo ukilinganisha na wanaume.


Na kwa sababu ya hili jambo, wanawake mara nyingi huhakikisha kuwa wanawazungusha wanaume mpaka ule wakati atapata anayemfaa. Wanafanya hivi ili kuangalia iwapo mwanaume lengwa anaweza kukeep mwendo wake. Anakupima iwapo unafaa kutoka deti na yeye. Wanawake hawawezi kukuambia moja kwa moja kuwa wanakupenda, badala yake wao hutumia ishara fioa ili ugande kwake.

Ishara zenyewe za kutaka umfukuzie ni kama fuatazo:

#1 Anakuwa mpole na mkali wakati sawia. Wanaume wengi washakumbana na mwanamke ambaye anakasirika na kuwa mpole wakati sawia. Ni ule wakati ambapo anaonyesha dalili ya kuwa rafiki yako na pia anaanza kukurushia mistari lakini wewe kwa upande wako ukijaribu anakufokea na kukukaa mbali na kukuona kama nuksi ghafla.

Ukiona jambo kama hili linakufanyikia usiwe na wasiwasi. Mwanzo shika virago vyako uende zako. Kwa akili yake hajakukasirikia bali anajaribu kukupa ishara ya kuwa anataka umfukuzie.

#2 Anajibu mesej zako haraka kama fastjet. Wakati mwanamke anajibu mesej zako haraka sana wakati wowote ule wa siku basi hio ni ishara ya kuonyesha kuwa anataka kuskia zaidi kutoka kwako. Inamaanisha kuwa amependezwa na wewe na anataka uendelee kuwasiliana na yeye mara kwa mara.

#3 Yuko tayari kukubali mialiko yako. Kama mwanamke hataki stori zako, basi kwa kawaida kwa haraka ukimwambia umtoe out ama matembezi atakataa. Mara nyingi atakwambia kuwa yuko busy muda wote na hana nafasi ya kutoka out na wewe. Lakini, kama kuna mwanamke ambaye anakuzimia na anataka umfukuzie, atatafuta njia ya kuhakikisha kuwa anakuwa na nafasi ya kuitikia mialiko yako, hata kama ni kuvunja mipango yake ya wikendi.

#4 Anakuwa makini na mwonekano wake anapokuwa na wewe. Utamshika pale wakati amevalia mavazi ya kawaida tofauti na vile ambavyo huvalia mkiwa nyinyi wawili. Kuvalia urembo ambapo kunaonekana si eti anavaa ili ajifurahishe, la. Huwa anavalia hivyo ili kuteka atenshen yako. Hivyo ni wewe tu unangojewa uchukue hatua ya kubadilisha kila kitu.

#5 Anakuwa na mazungumzo ya maana mnapokuwa pekeenu. Hapa haimaanishi atazungumzia kuhusu udaku wa Wema Sepetu ama Vera Sidika, bali mwanamke ambaye anataka afukuziwe atazungumza na kugusia maisha yake ya kibinafsi kwa kuongea maswala muhimu. Anataka uwe na shauku ya kutaka kujua maisha yake ya ndani ama kuzimu.

#6 Anakutesa. Kutesa kunaweza kumaanisha mambo mengi na tofauti tofauti. Lakini kama unaona anakutesa kiasi, ni ishara ya kuonyesha kuwa yuko huru na wewe na unapaswa kujiandaa kukeep company tofauti na vile ambavyo umezoea, yaani anakukaribisha katika himaya yake ya binafsi. Hii inachukuliwa kama hatua moja kuu ya kusongea mbele katika approach yako.

#7 Anawasiliana na wewe kama umekatiza mawasiliano. Kuna wakati mwingine kumfukuzia kunachosha na unaamua kutulia kiasi. Na mara kwa maajabu ya Musa, unaona mambo yameenda sengemnege, na unamwona anaaza kuanzisha mawasiliano na wewe.

Huu si uchawi bali ni ishara ya kuonyesha kuwa ameingiwa na wasiwasi wa kuwa unashindwa. Hivyo anakupa ishara fioa kukuambia kuwa unapaswa uendeee kumfukuzia.

#8 Anakuwa na tabia isioeleweka wakati mwingine. Wakati mwingine mwanamke atakupa jibu usilolitarajia kamwe, ama wakati mwingine unajiona uko pekeako ukiwa na yeye. Kuonyesha tabia tata kwa mwanamke huwa ni mbinu ya kijanja ambayo wanawake hutumia ili kukupima iwapo unaweza kutoboa katika maisha yao. Pia huongeza romance ndani yake.

#9 Analilenga lile swali kuu. Wakati mwingine inaweza kufikia ule wakati wa kumuuliza swali la iwapo yuko tayari kuingia katika uhusiano na wewe ili muwe kitu kimoja.

Na wakati unapomuuliza swali hilo analenga, ama anajaribu kuleta mada nyingine tofauti. Si eti kuwa hataki kukujibu, la. Tunajua mwisho atakubali kukujibu lakini kwanza atajaribu kukuzungusha huku na kule ili kujipa time. Hili ni jambo la kawaida kwa wanawake so kuwa na subra kiasi.

#10 Hatangamani na wewe sana lakini anakwambia kuwa anakumiss. Hii wakati mwingine inachosha akili. Ukimwambia mtoke out pamoja anaweza kukuambia yuko busy na hana nafasi lakini anakwambia kuwa anakumiss. Kama ni kweli anakumiss basi anapaswa kutangamana na wewe mara kwa mara. Hii ni ishara ya kuonyesha kuwa anataka umfukuzie.

#11 Anakuuliza kama umemmiss. Anapenda sana kukuuliza swali hili mara kwa mara. Njia nzuri ya kumjibu ni kumwambia kuwa unammiss na unataka utoke out na yeye. Kumwambia hivi kutamwacha na bila jibu bali kukubali.

#12 Anajifanya mgumu kumpata. Wanaume huwa na uhusiano wa penda-chukia kwa wanawake ambao wanajifanya ni wagumu. Mara nyingi kile wanachosema huwa hawanaanishi walichonacho akilini mwao. Anaweza kusema kuwa hajavutiwa na wewe lakini maneno na miondoko yake inasema tofauti. Ukiona mwanamke anaonyesha tabia kama hizi basi jua kuwa anataka umfukuzie.

Je ushakumbana na mwanamke aina hii? Kama ndio basi usikate tamaa. Tia bidii mwisho utafualu.



No comments:

Jiunge na jamii yetu ya Facebook/App yetu ili uweze kutangamana na members na readers wetu wa Nesi Mapenzi ama ujitafutie mpenzi HAPA

Powered by Blogger.