Sababu 9 Kwa Nini Watu Hujipata Wamependa


Mapenzi ni nini? Kuuliza swali hili kwa mtu yeyote atakupa majibu yasiyokuwa na kikomo. Mapenzi ni dhana pana ambayo kila mtu anakuwa na mtizamo tofauti wa kueleza. 

Kiufupi mapenzi ni jambo lisiloeleweka, jambo lisilo na mwisho. Na kwa kuwa mpenzi wako anachangia pakubwa katika kuyaendeleza mahusiano yenu yawe marefu ya kufaana, furaha, na hata kukuwezesha kuwa na maisha bora, tumekuja na tafiti tulizilokusanya kukupa sababu za kisaikolojia ambazo zinachangia wapenzi wawili wapendane.

Ok, kabla ya kuorodhesha orodha nzima je  ulikuwa ukijua kuwa homoni zako, maslahi, na hata sura ya mzazi wako inachangia pakubwa kwa kumchagua yule ambaye atakuwa mpenzi wako?

Zama nami...


Sababu za kwa nini watu huangukia katika mapenzi


1. Kama mnafanana ile sana
Tafiti zinaonyesha ya kuwa ile dhana ya kuwa "watu tofauti huvutiana" haina msingi. Badala yake wale watu ambao wanagawa mambo mapana, kama vile hulka, wana urahisi wa kuhisi sawa katika maisha yao ya kila siku. Utafiti huu uliweza kuthibitishwa na Gian Gonzaga, mwandishi mkuu katika eHarmony. Utafiti huu ni wa uhakika kwani katika maisha ya kawaida  ya mapenzi, iwapo wapenzi wanagawa hulka, moja maisha yao ya kimapenzi huwa marefu na ya kufaana.

2. Kama unafanana kama mzazi wake
Kulingana na mwana saikolojia David Perrett kutoka chuo kikuu cha St. Andrews amegundua ya kuwa watu huvutiwa na jinsia ile nyingine ambayo wana nywele na rangi ya macho ambayo ni sawia na ya mzazi wake wa ile jinsia tofauti. Pia katika tafiti yake amegundua kuwa "wanawake ambao walizaliwa na wazazi ambao ni 30+ hawavutiwi sana na  wanaume vijana ila wale wakubwa, tofauti na wanawake waliozaliwa na wazazi wadogo." Katika wanaume, Perrett alikiri kuwa kuchagua mpenzi kisura kwa mwanaume kunachangiwa pakubwa na umri wa mzazi wake wa kile. [Soma: Mbinu ya kuwa 'classic' kutongoza wanawake]

3. Kama unanukia ipasavyo
Katika mapenzi, chuo kikuu cha California kilifanya utafiti kikagundua ya kuwa mwanamke ambaye ameingia siku zake ya uzazi (ovulating) huwa wanapenda na kuvutiwa sana na harufu ya tsheti iliyovaliwa na mwanaume ambaye ana kiwango kikuu cha homoni za testosterone. Pia wanawake hao hao walikiri kupenda wanaume ambao wana taya ndefu.

4. Kama utawacha mikono yako na kifua chako wazi
Kuweka mikono yako ndani ya mifuko na kuyaweka mabega yako ndani unatoa ishara ya kuwa hujiskii kuongea. Lakini iwapo unaongea huku mikono yako umeiweka wazi na kusimama wima kifua mbele kunaonyesha ya kuwa ukotayari kwa lolote lile.

5. Kama mtaangaliana machoni kwa dakika mbili
Wakati mwanasaikolojia Joan Kellerman katika chuo kikuu cha Massachusetts alipowaagiza wanafunzi 72 wawili wawili waangaliane kwa dakika mbili mfululizo, waliripoti kuongezeka kwa hisia za upendo na mapenzi kwa huyo mwenzake. Hii ni idhibati tosha ya kuonyesha ya kuwa muda mrefu wa kuangaliana macho kunaweza kukakuunganisha na mtu na hata kuchangia hisia za mapenzi. [Soma: Matumizi ya macho kutongoza]

6. Kama unamiliki mbwa
Katika majaribio katika chuo kikuu cha Michigan, wanawake hupenda kusoma tabia za wanaume. Iwapo kuna habari ambayo inahusisha mwanaume ambaye anamiliki mbwa, wanawake wanampa kiwango cha juu cha uhusiano mrefu wa kuvutia. Hii ni kwa sababu watafiti walivumbua ya kuwa umiliki mifugo wa nyumbani inaweza kuwa ishara ya mtu ambaye ni mmakinifu na mwenye kuwa na hulka ya kupenda kujitweka majukumu katika mahusiano.

7. Kama unacheza mziki
Watafiti katika nchi ya Ufaransa wamegundua kuwa uhusisho wa mziki kunahusiana na uchaguzi wa mapenzi. Katika majaribio, mwanaume aliyebeba gita ama begi la mchezo aliuliza wanawake 300 namba zao za simu. Mwanaume aliyebeba gita aliweza kupewa namba nyingi zaidi kuliko alipobeba begi la mchezo.

8. Kama utavalia nguo nyekundu
Katika utafiti uliofanywa Slovakia, wanawake ambao walivalia nguo za rangi nyekundu walifanikiwa zaidi katika mchezo wa kufanya mapenzi. Hii ilichangiwa pakubwa na ishara ya kuwa nguo nyekundu wanawake wengi wanaitumia kama njia ya kuwavutia wanaume wenye uwezo. [Soma: Mbinu ya kujeuza mwonekano wako uvutie wanawake]

9. Kama una nywele flani katika uso wako
Katika utafiti wa mapenzi uliofanywa nchini Australia uligundua kuwa wanawake huvutiwa zaidi na wanaume ambao wana ndevu wastani katika uso wao. Waligundua kuwa mwanaume mwenye ndevu nyingi ama ambaye amenyoa uso mzima hawavutii kwao. Pia watafiti waligundua kuwa mwanaume mwenye nywele nyingi zaidi, huonekana na wanawake kuwa kiume zaidi.


1 comment:

  1. Mi nilikuwa naomba ushauri wenu kabla sijaingia katika mahusiano na mtu bila ya kujipanga kikamilifu

    ReplyDelete

Jiunge na jamii yetu ya Facebook/App yetu ili uweze kutangamana na members na readers wetu wa Nesi Mapenzi ama ujitafutie mpenzi HAPA

Powered by Blogger.
##valentine ##valentine