Jinsi Ya Kumuapproach Mwanamke Kwa Kutumia Michongo


Kujifundisha jinsi ya kumuapproach mwanamke kwa mara ya kwanza si jambo gumu la kufanya kama utafuata kanuni na masharti na kuyahifadhi baadhi ya michongo kwa moyo. Michongo ni maneno ya kwanza ambayo mtu hutumia kuanzisha maongezi na mwanamke. Maneno haya ndio mara nyingi hutumiwa na wanaume mara yao ya kwanza wanapomshobokea mwanamke. Ukiitumia vizuri michongo itakupa wewe nafasi ya kumvutia mwanamke kwa uharaka zaidi.

Ingawa wanaume wengi hutegemea zaidi bahati ama kukosa, hauwezi kamwe kufaulu kumridhisha mwanamke iwapo hujui kuipanga michongo yako vizuri pindi unapokutana na mwanamke unayemzimia kwa mara ya kwanza.

Ok. Kukusaidia kujipanga vyema,  tumeweza kuiorodhesha baadhi ya michongo iliyowazi na iliyofunge na jinsi ya kuitumia.

Aina ya michongo -wazi na funge

Unaweza kumuapproach mwanamke bila wasiwasi kwa kutumia michongo aina mbili -wazi na funge. Michongo ile mizuri zaidi inakuwezesha wewe kuonekana kujiamiani, mcheshi na kuonekana mtu anayevutia zaidi kuwaliko wengine walioko karibu nawe.

Ijapokuwa michongo iliyowazi inahitaji mtu mwenye kujiamini kwa kiasi cha juu, michongo funge inaweza kutumika na yeyote yule bora tu ufuate masharti ya kuitumia.

Michongo iliyofunge
Aina hii ya michongo ni rahisi kuitumia kwa mwanamke na si rahisi kwake kuelewa kama unatumia maneno kama hayo ukiwa na ajenda fulani. Michongo hii ni kuanzia matukio, kumsifu ama kuangazia mazingira. Kila aina ya michongo hii ina manufaa yake na pia upungufu wake kiasi fulani kulingana na mazingira ambapo yanatumika. [soma: Hatua za kufanya kama mwanamke anakataa kujibu texts zako]

1. Matukio
Aina hii ya michongo ni rahisi kuikumbuka na ukiitumia kwa mwanamke atakupa atenshen yake automatic. Michongo hii hutumika ili kutaka atenshen ya mwanamke kwa kujaribu kumuuliza maswali ambayo yanalingana na mazingira aliyeko.
Baadhi ya aina ya michongo iliyofunge ni kama:
"Unaweza kujua wakati gani gari lingine la abiria linaweza kufika hapa?"

"Je unajua sehemu nzuri ambayo mtu anaweza kujiinjoy katika huu mji?"

"Nlikuwa nataka kuvuta sigara lakini kibiriti changu sikioni, naweza kuomba chako?"

"Nilikuwa sijamaliza kuandika maswali ya mwalimu kwa ubao, unaweza kunisaidia kitabu chako?"

2. Kumsifu
Aina hii ya michongo inakaribiana na ile ya wazi lakini kwa mpango flani inazuia kumfanya mwanamke kuelewa ajenda yako kwa uharaka. Michongo hii inafaa zaidi wakati ambapo inatumika katika vilabu, sehemu za kujivinjari ama sehemu yeyote ile ambayo unaona inaweza kutumika.
Kabla hujamsifu, ni lazima uhakikishe ni kwanini unamsifu manake mara nyingi unapomsifu mwanamke kuhusu jambo fulani atataka kujua kwa nini unammiminia sifa kama hizo.
Baadhi ya michongo ya kumsifu ni kama vile;
"Dress uliyoivaa imekupendeza, yaani imekufanya kuonekana mfano wa malaika"

"Una pozi lengine ajab, lazima wewe ni dansa flani"

"Nimependezwa na mtindo wako wa nguo na umbo lako, umetoklezea"

Ujanja wa kutumia aina hii ya michongo ni kuhakikisha unacheza na tabia na umbo lake, hakikisha kuwa unajaribu kumchunguza ili kupata mambo ambayo anayapenda kumhusu yeye. Usisahau ya kuwa utafiti umebainisha kuwa wanawake hupenda sana kusikia wakisifiwa.

3.  Kuangazia mazingira
Kulingana na mazingira, unahitaji kuifahamu sanaa ya kuingia katika akili ya mwanamke na kufahamu kile ambacho anafikiria. Ukifahamu kile ambacho anafikiria, itakuwa ni jambo jema zaidi.
Kwa mfano,  kama mwanamke anajaribu kusoma lakini kila dakika anasumbuliwa na jambo fulani, unaweza kumuuliza: "Si inaonekana ni vigumu zaidi kusoma wakati ambapo jua ni kali zaidi huko nje?"

Kama umekutana na kundi la wanawake na ungetaka kuanza kuongea nao, unaweza kuwaapproach halafu useme "Nyinyi wanawake mnaonekana mnaenjoy sana na wenye nishati, kwani kitu gani kinachoendelea ambacho nakikosa?"

Pia kama kuna mwanamke unayemzimia na hujawahi kuongea na yeye unaweza kumwambia "happy birthday"

Michongo iliyowazi
Kama wewe una confidence na unajiamini kuwa unaweza, basi njia yako ya kutumia ni michongo iliyowazi. Kumbuka kuwa kama wakati wowote utaonyesha unyonge katika sauti yako juwa ya kwamba michongo yako itaanguka hapo hapo na utajiaibisha mwenyewe. [soma: Jinsi ya kumfanya mwanamke akutamani]

Kutumia michongo iliyowazi itakuwezesha wewe kukupatia matokeo ya haraka kwa sababu ni kuwa wanawake hupenda wanaume ambao wanajiamini kwa mambo wanayoongea na kufanya. Kama mwanamke ataonyesha dalili zozote za kutaka kuongea nawe kwa njia ya miondoko ya mwili, basi unafaa kutumia michongo iliyowazi.
Baadhi ya michongo iliyowazi ni kama vile:
"Unaoneka mrembo, unaweza kuniruhusu nitake kukujua zaidi?"

"Nilikuwa nimekuona kutoka upande ule mwingine wa nyumba na nikaamua kuja kukusalimia, bila hivyo ningeishi kujutia kukosa kumjua mwanamke mrembo zaidi maishani mwangu"

Mwisho ni kuwa hakikisha kuwa baada ya kutumia hii michongo kupata atenshen ya mwanamke, hakikisha unaendeleza maongezi yenu. Jaribu kupata kulijua jina lake halafu ujibidiishe kulitumia kila wakati, lazima atapenda.

Usisahau kutumia sanaa za kutongoza kwa kujua vitu ambavyo mnagawa interest pamoja, jinsi ya kumfurahisha na kadhalika. Hii utamfanya apendezwe na wewe na mudan usiomrefunatakuzoea.


No comments:

Jiunge na jamii yetu ya Facebook/App yetu ili uweze kutangamana na members na readers wetu wa Nesi Mapenzi ama ujitafutie mpenzi HAPA

Powered by Blogger.